WANANCHI WAANDAMANA POLISI LAMADI WATOTO KUPOTEA




Polisi na wananchi

Shughuli za wananchi wa Kata ya Lamadi wilayani Busega, mkoani Simiyu, zimesimama tangu asubuhi, baada ya wananchi kuandamana katika kituo cha polisi cha Lamadi kwa madai ya kukithiri kwa matukio ya watoto kupotea katika mazingira yasiyojulikana.

Hali hiyo imepelekea wananchi kufunga barabara kuu, inayounganisha mikoa mitatu ya Mwanza, Simiyu na Mara, huku wakiyashambulia magari yanayopita barabani kwa mawe wakidai wamechoshwa na matukio hayo.

Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Simiyu, inayoongozwa na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Simon Simalenga, imefika katika eneo hilo na kuimarisha usalama kwa kuwatawanya wananchi hao kwa kupiga mabomu ya machozi.

Chanzo- EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post