DEREVA,UTINGO NA ABIRIA WATEKETEA KWA MOTO AJALI MALORI KUGONGANA USO KWA USO KAHAMA


Dereva,Utingo na abiria wamefariki dunia kwa kuteketea kwa moto huku wengine watatu wakijeruhiwa katika ajali iliyohusisha Malori mawili kugongana uso kwa uso katika eneo la Manzese wilayani Kahama mkoani Shinyanga huku chanzo cha ajali hiyo kikitajwa kuwa uzembe na Mwendokasi.
Inaelezwa kuwa ajali hiyo imehusiha malori mawili ya mizigo  ambapo baada ya kugonga uso kwa uso  yalianza kuwaka moto  na kusababisha vifo vya dereva, utingo na mtu mwingine ambaye anaidawa kuwa ni abiria ambapo jina lake bado halijafahamika.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga SACP Janeth Magomi amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambayo imehusisha Malori mawili ya Mizigo Namba T 854 DBY lenye tela namba T 180 DVH na Lori namba T 195 EEY lenye tela namba T 811 DYU. #Malunde 1 blog Updates

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post