WAJIPANGA KUGAWA MBEGU CHOTARA ZA ALIZETI MSIMU UJAO KWA MFUMO WA RUZUKU

Alizeti aina ya Sunbloom mbegu chotara zitakazosambazwa Msimu ujao kwa bei ya ruzuku na Wakala wa Mbegu


Wakala wa Mbegu za Mazao wamejipanga kugawa mbegu chotara za alizeti kwa wakulima kwa mfumo wa ruzuku.

Tayari tani  zaidi ya 600 zipo na ziko kwenye mchakato wa kuziandaa ili ziingie sokoni. 

Kaimu meneja masoko wa Wakala wa mbegu za mazao,Edward Angolile Mbugi amesema mbegu hizo zimeagizwa kytoka nchini India na aina hii ya mbegu inaitwa SUN BLOOM. Itauzwa kwa shilingi 10,000 kwa kilo.

 Hivyo wananchi walichangamkie ili kupunguza pengo la upungufu wa mafuta ya kula.

Nao wadau wengine wa kilimo cha alizeti wamekuja na maonesho ya mbegu chotara na kuwataka wakulima wa mikoa ya Singida na Dodoma kwenda kujifunza kilimo bora'' na chenye tija cha alizeti kwenye maeneo ya mashamba darasa yaliyoandaliwa kwenye viwanja hivyo vya Nzuguni.

Afisa Ugani wa Halmashauri ya Singida  anahamasisha wakulima kutumia mbegu ya Aguara6 na SuperSun ambazo zimeonesha kufanya vizuri na kuwa na sifa tofauti ya kuwa na kichwa kikubwa na mbegu zilizojaza, nzito na zenye mafuta mengi.

Amewataka wakulima wa zao la Alizeti kufuata kanuni za kilimo bora'' na kuweka mbolea kwenye zao  hilo kwani wengine hawatumii mbolea kwenye kilimo cha alizeti matokeo yake wanavuna gunia moja kwa ekari.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post