BRELA YAJIPANGA KUANZA KUWAPA NEMBO YA UTAMBULISHO WAKULIMA


Na Dotto Kwilasa,Malunde Blog 1 Dodoma

Afisa usajili wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) Gabriel amesema wakala huo umejipanga kuanza kuwasajili Wakulima kwa kuwapa nembo ambayo itawatambulisha kibiashara.

Hayo yameelezwa leo Agosti 4,2024 kwenye maonesho ya Wakulima Nanenane Jijini hapa wakati akizungumza na Waandishi wa habari na kueleza kuwa Wakala huo unashughulikia mambo mengi kwa wakulima nchini ikiwemo Usajili wa Biashara.

Amesema BRELA inawasaidia wakulima kusajili biashara zao rasmi ili kuwa na usajili wa kampuni, ushirika, au biashara ndogo ndogo zinazohusiana na kilimo.

"Usajili huu unasaidia kupata haki ya kufanya biashara na kufanya biashara kwa ufanisi zaidi,usajili wa alama za Biashara ikiwa ni pamoja na kutoa huduma za kusajili alama za biashara (trademarks) ambazo zinaweza kuwa muhimu kwa wakulima kulinda jina la bidhaa zao na alama zinazotumika katika masoko na kutoa Leseni na Vibali, "amesema

Mbali na hayo amesema BRELA hutoa huduma hizo ili kuhakikisha biashara za kilimo zinakubalika kisheria ikiwa ni pamoja na kutoa huduma za ushauri kuhusu jinsi ya kufuata taratibu za kisheria katika biashara ya kilimo, ikiwa ni pamoja na kanuni za usajili, sheria za biashara, na masharti ya leseni.

"Kwa hivyo, BRELA inachangia katika kuhakikisha kuwa wakulima wanapata huduma zinazohitajika ili kuendesha shughuli zao za kilimo kwa njia rasmi na kisheria, " amefafanua Afisa usajili huyo.
Kwa upande mwingine Wakala huo hushughulikia Kampuni za Umma,Kampuni zinazoshiriki soko la hisa,Kampuni za Kibinafsi na Kampuni zinazomilikiwa na watu wachache.

"Kwa wakulima na wafanyabiashara wote hakikisheni mmefanya utafiti wa kina kuhusu kampuni unayotaka kuisajili,angalieni pia Kampuni mnazotaka kuingia ubia nayo,angalia historia yake, hali ya kifedha, na sifa zake," Amesema

Kuhusu kufanya Mkataba wa Ubia amesema mkataba wa ubia unaoeleza masharti ya ushirikiano unapaswa kuandaliwa mapema ikiwa ni pamoja na majukumu ya kila upande, na uwajibikaji.

Amesema, "Mkataba huu unapaswa kuwa wa kisheria na unaweza kuwa na huduma za kisheria kuhusiana na mgogoro wa baadaye.Kusajili na Kuandikisha: Hakikisha kuwa ubia wako umeandikishwa rasmi na BRELA au mamlaka husika.

"Ili biashara ifanyike bila usumbufu fahamu majukumu yako ya kisheria na yale yanayohusu ubia,hii ni pamoja na kutambua jinsi ya kulipa kodi, leseni, na vibali vya biashara lakini pia mfumo mzuri wa mawasiliano na usimamizi wa mahusiano ya kibiashara unapaswa kuzingatiwa ili kuondoa migogoro na kuboresha ushirikiano,"amesisitiza

Amesema BRELA ikiwa ni shirika la serikali linalosimamia usajili wa biashara, kampuni, na mashirika lengo lake ni kurahisisha mchakato wa usajili, kutoa huduma za leseni, na kuhakikisha kuwa biashara zinakubaliana na sheria na taratibu za nchi.

"Huduma kuu zinazotolewa na BRELA ni pamoja na Usajili wa Kampuni,Kusajili kampuni, mashirika, na ushirika ikiwa ni pamoja na kutoa mwongozo na ushauri kuhusu sheria za biashara na taratibu za kisheria, " amesema

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post