DK. NDUNGULILE MGOMBEA NAFASI YA MKURUGENZI MKUU SHIRIKA LA AFYA DUNIANI KANDA YA AFRIKA






Na Mwandishi wetu

Mgombea nafasi ya Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani Kanda ya Afrika Mheshimiwa Dkt. Faustine Ndugulile akijinadi mbele ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa 74 wa WHO leo Agosti 27, 2024 unaofanyika katika Jiji la Brazzaville nchini Congo.

Dkt. Ndugulile amesema vipaumbele vyake katika kazi hiyo endapo atachaguliwa kuwa ni kuhakikisha Watu wanapata haki ya kupata huduma bora za afya; Kuboresha utayari wa nchi za Afrika katika kukabiliana na majanga ya magonjwa ya mlipuko, Kuimarisha uwajibikaji ndani ya WHO kanda ya Afrika pamoja kuimarisha mawasiliano baina ya nchi wanachama katika masuala ya Afya.

Zoezi la uchaguzi wa Mkurugenzi Mkuu wa WHO Kanda ya Afrika unafanyika leo kupitia Mawaziri wanaoshughulikia masuala ya Afya Afrika chini ya Shirika la Afya Duniani.





Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post