DKT MWASE AHIMIZA UPANDAJI WA MITI NA KUISIMAMIA KATIKA UKUAJI WAKE MPAKA IWE MIKUBWA

Mkurugenzi wa wa Shirika la Taifa la Madini Tanzania (STAMICO) Dkt Venance Mwase akipanda miti katika eneo la Amboni Jijini Tanga lililoratibiwa na Wanawake na Samia Mkoa wa Tanga lililokwenda sambamba na kutambulisha Nishati Safi mbadala ya  Rafiki Briquettes.

Mkurugenzi wa wa Shirika la Taifa la Madini Tanzania (STAMICO) Dkt Venance Mwase akipanda miti katika eneo la Amboni Jijini Tanga lililoratibiwa na Wanawake na Samia Mkoa wa Tanga lililokwenda sambamba na kutambulisha Nishati Safi mbadala ya  Rafiki Briquettes.

Mkurugenzi wa wa Shirika la Taifa la Madini Tanzania (STAMICO) Dkt Venance Mwase akipanda miti katika eneo la Amboni Jijini Tanga lililoratibiwa na Wanawake na Samia Mkoa wa Tanga lililokwenda sambamba na kutambulisha Nishati Safi mbadala ya  Rafiki Briquettes.

Mkurugenzi wa wa Shirika la Taifa la Madini Tanzania (STAMICO) Dkt Venance Mwase kulia akikabidhiwa miti kabla ya kuupanda katika eneo la Amboni Jijini Tanga lililoratibiwa na Wanawake na Samia Mkoa wa Tanga lililokwenda sambamba na kutambulisha Nishati Safi mbadala ya  Rafiki Briquettes.


Na Oscar Assenga, TANGA

 

SHIRIKA la Madini la Taifa (Stamico) limesema kwamba agenda yao katika kutunza mazingira sio kupanda miti na kuiacha bali ni kuhakikisha wanaisimamia katika ukuaji wake mpaka inapokuwa mikubwa.

 

Kauli hiyo ilitolewa leo na Mkurugenzi wa wa Shirika la Taifa la Madini Tanzania (STAMICO) Dkt Venance Mwase wakati akishiriki zoezi la upandaji wa miti katika eneo la Amboni Jijini Tanga lililoratibiwa na Wanawake na Samia Mkoa wa Tanga lililokwenda sambamba na kutambulisha Nishati Safi mbadala ya  Rafiki Briquettes.

 

Alisema katika agenda hiyo wanazuia pia kukata miti na ili kuizuia lazima kuwa na nishati safi mbadala ya Rafiki Briquettes ambao ni ubunifu uliofanya na shirika hilo katika kuhakikisha suala la utunzaji wa mazingira linapewa umuhimu mkubwa

 

“Lakini suala la nishati safi ya kupikia ni agenda ya Rais hivyo niwapongeza wanawake na Samia mkoa wa Tanga kwa kuunga mkono agenda hiyo hivyo tutaendelela kuwaunga mkono “Alisema

 

Aidha alisema kwamba wanawajibu wa kutunza mazingira na kufanya hivyo lazima waangalie nini kinafanya mazingira yanaharibika wananchi wengi bado hawana nishati mbadaa bado wanatumia kuni na mkaa ambao unatokana na miti hali ambayo inawafanya kwenda kukata miti ili kupata nishati ya kupikia.

 

Alisema kwamba programu yao hiyo inakwenda na vitu viwili kwanza hiyo miti inayokatwa wanataka wahamasishe ili ipandwa ndio kitu wanachokifanya  ili kuzuia isikatwe wananchi lazima apike na ale ndio maana wamekuja hiyo nishati mbadala ya kupikia ya Rafiki inatokana na ubunifu na utafiti uliofanywa na shirika la madini la Taifa (Stamico) .

 

Alisema ili kuhakikisha wanapata nishati mbadala kwa ajili ya wananchi  ambayo ni rafiki kwa matumizi,mazingira na bei kutokana na vipato vyao kwa hiyo wameitamblisha hiyo bidhaa mkoani Tanga .

 

“Kimsingi utafiti umekamilika na uzalishaji umeanza na namna ya kuuza hiyo bidhaa kundi la wanawake na samia ndio watakuwa wauzaji watakuwa wanazalisha viwandani na watakauokuwa wanaiuza na kuhamasisha matumizi hayo watakuwa ni wakina mama  kwa sababu wanakina mama ndio wanaathirika zaidi na utafutaji wa nishati na uchafuzu wa mazingira maana wanasema uchungu wa mwana ni mzazi”Alisema

 

Alisema kwamba ndio sababu ya kuwapa fursa hiyo ili waunge mkono agenda ya Rais ya mazingira na nishati mbadala ya kupikia lakini hiyo bidhaa impe uchumi huku akieleza kwa kuisambazaji haitakuwa kazi ya bure ni ya kibiashara na watawawesha kuwa na kontena na eneo la kuuzia na kuwatangazia na kwenye matukio mbalimbali kama hayo watawasaidia ili kuhakikisha wameweka hamasa kwa wananchi wote waache na kukuata miti na watumie nishati safi mbadala.

 

 

 

“Agenda ya mazingira ni ya Rais hivyo mmeichagua jambo sahihi kwa wakati sahihi tutawasapoti tunatunza mazingiwa kwa vizazi vya sasa na vijavyo na mazingira yamekwenda kwenye kuingia kwenye ajira ya uchumi “Alisema

 

Hata hivyo alisema mazingira yanapochafuliwa yatakuja kuathiri baadae na watashindwa kulima, kupata hewa nzuri huku akiwataka kulifanya zoezi hilo liwe endelevu na wanapopanda miti lazima waitunze.

 

Awali akizungumza katika zoezi hilo Mwakilishi wa wanawake na Samia walimshukuru Dkt Mwase kwa kuja Tanga kuungana nao katika zoezi hilo kutokana na kwamba wanawake na samia wapo mikoa 25 hapaa nchini lakini ameweza kuitika kuwa pamoja.

 

“Kwa pamoja huo ni muendelezo wamepanda miti leo ili waweze kutumia mkaa mbadala hivyo wanawake na samia wana deni la kwenda kuhamasisha wananchi jinsi gani ya kuacha kukata miti na kutumia kuni katika kupika na kueleza athari zake  kwa kutoa elimu kwa wananchi ili fursa inapokuwa imekamilika wawe na uelewa wa pamoja”Alisema  

 

Naye kwa upande wake Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Bonde la Mto Pangani Michael Buli  alisema kwamba katika kampeni hiyo ya wanawake na samia mkoa wa Tanga ya kutunza mazingira watakuwa nao bega kwa bega kushirikiana katika kutunza mazingira  na vyanzo vya maji katika maeneo yote yanayostahili.

 

Michael ambaye ni katibu wa Jumuiya ya watumiaji Maji wa Bonde Zigi chinialisema kqa sababu mazingira yamekuwa hatarishi sana na wakiendelea hivyo miaka 10 ijayo Tanzania itaendelea kuwa ya kijani na kama watakuwa nyuma basi Tanzania itakuwa nyeusi .

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post