MBUNGE MTATURU AMWAGA VIFAA VYA UJENZI MANG'ONYI


MBUNGE wa Singida Mashariki Miraji Mtaturu,amekabidhi mifuko 100 ya saruji na mtofali 1,000 kwa ajili ya kuanzisha ujenzi wa maabara za sayansi katika Shule ya Msingi Mang'onyi Shanta ikiwa ni kutimiza ahadi yake aliyoitoa wakati wa mahafali ya kidato cha nne mwaka jana 2023.

Msaada huo ameukabidhi Agosti 4,2024,akiwa katika muendelezo wa ziara yake ya kusikiliza kero za wananchi,kutoa mrejesho wa Bunge la Bajeti 2024/2025 na kuhamasisha uchaguzi wa serikali za mitaa,vijiji na vitongoji 2024.

Akikabidhi msaada huo kwa Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Mohamed Khalid,Mtaturu amesema kukamilika kwa maabara hizi kutaondoa changamoto waliyokuwa wanaipata walimu kuwafundisha wanafunzi masomo ya sayansi kinadharia tu.

Akitoa shukrani kwa niaba ya shule,Mkuu huyo wa shule Mwalimu Khalid amemshukuru mbunge kwa kuendelea kuwashika mkono muda wote.

"Tunaomba utufikishie shukrani zetu kwa Rais Dkt Samia Suluhu hasaan kwa kutuletea Milioni 37 za kujenga darasa moja na matundu 6 ya vyoo,tunamshukuru sana,ahsante sana pia ndugu yetu Mtaturu kwa kutimiza ahadi yako,".amesema.

Makabidhiano hayo yameshuhudiwa na Mwenyekiti wa Bodi na wajumbe wake.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post