TIMU ZA NETIBOLI, KIKAPU ZA TANZANIA ZATAMBA FEASSSA 2024


Na Angela Msimbira UGANDA

Timu ya Netiboli ya Tanzania katika michuano ya Shule za Msingi na Sekondari ya Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (FEASSSA) imeibuka na ushindi kwa kuichapa timu ya Rwanda mabao 66- 32.

Katika mashindano hayo ya 22 yanayofanyika Mji wa Mbale nchini Uganda, mchezo huo umechezwa viwanja vya shule ya msingi Mukedea.

Kwa upande wa mpira wa Kikapu 5x5 Timu ya wavulana ya Tanzania imeichapa Uganda kwa mabao 77- 70, huku 3x3 ikipata mabao 13-10.

Timu ya Tanzania ya Mpira wa Mikono kwa wavulana imeonyesha uwezo wake baada ya kucheza na Kenya na kupata magoli 22-23.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post