RAIS SAMIA : WATUNZENI WATOTO TUSIJE KUSIKIA KESI ZA UJAUZITO, SITAKI KUSIKIA MSURURU WA WALIOPATA ZERO


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amezindua Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mchepuo wa Sayansi na Sanaa Namtumbo Mkoani Ruvuma iliyopewa jina la ya Dr.Samia Suluhu Hassan ambayo ujenzi wake umegharimu Shilingi Bilioni 4.6 leo September 27,2024.


Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Rais Samia amesema:
"Nizungumze kidogo na walimu, kwanza hongereni mwalimu mkuu hongera na walimu wenzio wote ambao mmekabidhiwa Watoto hawa. Ninalotaka kuongea nanyi ni kwamba tumewakabidhi Watoto wetu, mazingira ni mazuri lakini niwaombe sana ninyi ndiyo Mungu amewachagua kuwa na watoto hawa, naomba watunzeni”. 

"Lakini jingine niwatake Watoto wangu mliopata fursa ya elimu kuitumia vizuri sana nafasi hii. Sitaki nisikie shule hii ina msururu wa walipata zero, hawakupata vyeti sijui daraja la nne aaah aaah, na mmeniambia kwenye kupasi hakuna wasiwasi,” amesema  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.




Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post