BALOZI WA TANZANIA NCHINI UGANDA ARIDHISHWA KASI UJENZI MRADI WA BOMBA LA MAFUTA


 Na Hadija Bagasha Tanga

BALOZI wa Tanzania nchini Uganda Meja Generali Paulo Kisesa Simuli amesema kuwa asilimia 50 ya  mabomba yatakayotumika  kwenye mradi wa bomba  la mafuta linalotoka Hoima nchini Uganda hadi Chongoleani Tanga Tanzania  imeshakamilika hii ikiwa inazidi kuchochea kasi ya ujenzi kwa wakandarasi wa  pande zote mbili ambao mpaka sasa wamefikia hatua nzuri.

Meja Simuli amebainisha hayo wakati alipofanya ziara ya kukagua na kutembelea kituo kikubwa cha Chongoleani Mkoani Tanga  ambapo ameridhidhwa na kasi ya ujenzi inavyoendelea akiwapongeza wakandarasi wa vituo vyote vinavyopitiwa na mradi huo hapa nchini.

"Mabomba ambayo yameshaletwa yameshafikia nusu ya mabomba ambayo yatatandazwa kutoka  Chongoleani  mpaka Hoima tayari wameshafikia asilimia 50 mkandarsi amesema kuwa yakitandazwa yanaweza kufikia urefu wa zaidi ya Kilomita 700  na urefu wa kutoka hapa (Chongoleani) mpaka Hoima ni Kilomita 1443, kwahiyo ni matumaini yetu kwamba huu mradi utakamilika na hautalala", alisema Meja Simuli  na kuongeza . 

"Kwa hatua tuliyofikia nawashukuru na kuwapongeza sana wakandarasi wote, TPDC  pamoja na wizara ya nishati ambao jambo hili wamelishikia bango bila  kuwasahau wizara yetu ya mambo ya nje kwa kuendelea kudumisha mahusiano kwa nchi zote mbili ambayo yanatunufaisha katika nyanja ya kiuchumi" 

"Mradi ni nzuri , wa kimakakati na wa kimaendeleo  nimefika pale Kahama ambapo wanayafunika mabomba ili yaweze kutunza joto lakini pia kuna  pampu zimewekwa kwaajili ya kusukuma haya mafuta ziko kwenye hatua nzuri kila sehemu ambayo  nimeenda  linakopita bomba hii  kazi inaendelea vizuri. 

Aidha alisema kuwa kwa upande wa Uganda tayari jumla ya pampu 6 zitakazotumika kuvuta mafuta kutoka ardhini zimeshafungwa.

"Kule Uganda tayari wameshafunga pampu 6 za kuvuta mafuta kutoka ardhini kwa maana hiyo mradi huu kwa kutathmini unakwenda vizuri , nawapongeza sana Kambi hii ya chongoleani kwa kazi na juhudi ambazo wanaendelea kuzifanya  katika kuhakikisha matakwa ya Serikali yetu yanafikiwa", aliongeza Balozi Kisesa.

Awali akizungumza msimamizi wa Kambi ya Chongoleani Reni Bezian kupitia kampuni ya DOCG  amesema kuwa  tayari kufikia sasa wameshafikia asilimia 20 ya utekelezaji wa mradi kwa  ikiwa ni pamoja na ujenzi wa mapima manne yaliyopo kwenye hatua ya awali ambayo yatakuwa na uwezo wa kuhifadhia mafuta million nne lengo lao likiwa ni kukamilisha kabla ya Kambi zote zinqzopitiwa na mradi huo.

" Mpaka sasa tumefikia asilimia 20 kwa  ujenzi wa miundombinu inayopaswa kuwepo hapa Chongoleani na asilimia 60 kwa upande wa mapipa ya kuhifadhia mafuta tayari  tumeshaanza hatua ya awali lengo letu ni kukamilisha kwa wakati na sasa tunawekeza nguvu zetu zote kuhakikisha tunakamilisha lengo la mradi mpaka 2026", alisema Bezian.

Aliongeza kuwa wanaendelea kutekeleza matakwa ya maktaba ikiwa ni pamoja na utunzaji wa mazingira pamoja na kutoka ajira kwa wazawa ambapo mpaka sasa katika Kambi hiyo Kuna wafanyakazi 1011 zaidi ya 800 wakiwa ni wazawa  wakiwemo wenye ujuzi 573, wasio na ujuzi 284.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post