MIAKA 60 YA JESHI POLISI MORO WATOA MSAADA KWA WATOTO WENYE ULEMAVU


Na Christina Cosmas,  Morogoro 

Kuelekea kilele cha maadhimisho ya miaka 60 ya Jeshi la Polisi,  Askari Polisi Mkoa wa Morogoro wametoa msaada wa vitu mbalimbali kwa watoto wenye mahitaji maalum katika kituo cha kulelea watoto yatima cha MEHAYO kilichopo Mazimbu mkoani humo.

Aidha, akizungumza baada ya kukabidhi msaada huo kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP Alex Mkama ameitaka jamii kuendelea kuwasaidia watu wenye uhitaji hususani watoto yatima ili nao wajione ni sehemu ya jamii yenye kupendwa na kuthaminiwa.

Kamanda Mkama aliambatana na askari wa vyeo mbalimbali na kukabidhi msaada kwa watoto hao ikiwa ni sehemu ya majitoleo yao na hasa kuguswa na kundi hilo lenye uhitaji kwenye jamii.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post