RAIS SAMIA AFURAHISHWA NA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA SHULE YA WASICHANA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amezindua Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mchepuo wa Sayansi na Sanaa Namtumbo Mkoani Ruvuma iliyopewa jina la ya Dr.Samia Suluhu Hassan ambayo ujenzi wake umegharimu Shilingi Bilioni 4.6 leo September 27,2024.


Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Rais Samia amesema:
"Nimefurahishwa pia kwamba Watoto mmeniimbia wimbo mzuri san. Wimbo ulionihakikishia kwamba huduma zote zinapatikana. Na nimekwenda kuona bwalo tu, nimeona huduma zote zinapatikana. Kilichonifurahisha zaidi ni matumizi ya nishati safi ya kupikia. Huu ni mradi wangu nilioubeba kwa ajili ya wanawake wa Afrika".


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post