ELIMU KWA JAMII KIJIJI KWA KIJIJI DAWASA CHALINZE


Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) imeendelea na uelimishaji wa makundi mbalimbali ya kijamii juu ya utunzaji na uhifadhi wa Miundombinu ya maji, matumizi sahihi ya huduma ya Majisafi pamoja na kusikiliza changamoto za kihuduma kwa Wananchi wanaohudumiwa na Mamlaka.

Elimu hii imetolewa kwa Wananchi wa cha Kijiji Manga kilichopo Wilaya ya Handeni , Mkoani Tanga ambao ni wanufaika na utekelezaji wa Mradi wa Maji Chalinze awamu ya tatu uliokamilika kwa asilimia 100.

Afisa Maendeleo ya Jamii DAWASA Bi.Elizabeth Eusebius ametumia nafasi hiyo kutoa ufafanuzi wa hatua mbali mbali zinazochukuliwa na Mamlaka katika kuimarisha huduma ya maji katika Kijiji hicho ikiwa ni pamoja na kufunga pampu mpya na kuimarisha mfumo wa umeme wa njia tatu katika tenki la maji Tengwe.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post