TAMASHA KUBWA LA BIA TANZANIA, #SERENGETIOKTOBAFEST 2024, LIMERUDI TENA.


Mabibi na mabwana, Wapenda bia, Wapenda vibe, na wapenzi wa tamaduni za Kitanzania, Tamasha kubwa la Serengeti Oktoberfest lililokuwa likisubiriwa kwa hamu sana limerejea, na mwaka huu, UKUBWA NA UBORA wa #SerengetiOktobaFest2024 haukuwahi kutokea Kabla!.

Mwezi huu wa Oktoba, #SerengetiOktobaFest itakuwa sherehe kubwa itakayoangazia uhalisia wa Mtanzania na kuamsha uhai wa utamaduni wa Kitanzania kupitia mchanganyiko usiomithilika wa Bia, Vyakula na Utamaduni wetu.

Jiandae kwa tafrija ya kitamaduni isiyosahaulika itakayokuwa kivutio cha mwaka. Kama ilivyokuwa mwaka jana, tamasha liliadhimishwa kama tukio kubwa zaidi la bia la Afrika Mashariki, mwaka huu, Oktoberfest itafanya hivyo hivyo katika nchi tatu tofauti za Tanzania, Kenya, na Uganda.

Tamasha hili litaonesha utambulisho wa kipekee wa kitamaduni wa kila eneo kupitia onesho lililopangwa na likapangika la vyakula vya nyumbani, muziki na utamaduni, huku bia yako pendwa ya Serengeti ikitumika kama kiunganisho kinachotuleta pamoja.

Kaa tayari na endelea kutufuatilia kwenye Kurasa za mitandao ya kijamii ya bia yako pendwa ya Serengeti ili kujua tarehe na eneo kutakapowekwa historia nyingine kubwa yenye kutuunganisha Waasisi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Hatuna Jambo dogo na nikuhakikishie tu kuwa #SerengetiOktobaFest 2024 inatazamiwa kuongeza joto na kutuleta pamoja kwenye kusherehekea bia yetu pendwa, utamaduni na vyakula vyetu.

Andaa washkaji, tayarisha pamba zako za kitamaduni, na kaa tayari kwa tamasha hili lenye hadithi na simulizi zisizosahaulika ambalo litakufanya ufurahie Utanzania wa kweli.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post