ASAKWA NA JESHI LA POLISI TANGA KWA TUHUMA ZA KUMUUA MKEWE NA BINTI YAO WA KAZI

 


Na Oscar Assenga, TANGA


JESHI la Polisi Mkoa wa Tanga linamtafuta Alii Mohamed Bagidadi (60) mkazi wa Barabara ya 4 Jijini Tanga kwa tuhuma za kumuua mke wake Saira Ali Mohamed (50) na binti wa kazi anayejulikana kwa jina la Aisha (20) kwa kuwanyonga na kamba aina ya katani shingoni kisha kuwatoboa macho.

Akithibitisha kutokea tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga (ACP ) Almachius Mchunguzi alisema kwamba tukio hilo lilitokea Septemba 30 saa moja usiku na kwamba baada ya mtuhumiwa kufanya kitendo hicho alitorokea kusikojulikana.

Kamanda Mchunguzi alisema kwamba Jeshi hilo linatoa wito wa wananchi kushirikiana na nao kutoa taarifa mahali popote atakapoonekana ili akamatwe na sheria iweze kuchukua mkondo wake.

“Kwa sasa tunamtafuta  mtuhumiwa huyo lakini pia nitoe wito kwa wananchi kutoa taarifa mahali popote atakapoonekana ili akamatwe na sheria iweze kuchukua mkondo wake “Alisema Kamanda huyo wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga.

Hata hivyo aliwaasa wananachi kuacha kujichukulia sheria mkononi kwani kufanya hivyo ni kinyume cha sheria za nchi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post