BARAZA LA NCC LATAKIWA KUWA KIUNGANISHI CHA MENEJIMENTI NA WAFANYAKAZI

 

NAIBU Waziri wa Ujenzi Mhandisi Godfrey Kasekenya,akizungumza wakati akizindua Baraza la Wafanyakazi la Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) lililofanyika leo Oktoba 23,2024 jijini Dodoma.

Mwakilisha wa Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Bw.Mrisho Mrisho,akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Wafanyakazi la Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) lililofanyika leo Oktoba 23,2024 jijini Dodoma.
Afisa Mtendaji wa Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC), Dkt. Matiko Mturi,akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Wafanyakazi la Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) lililofanyika leo Oktoba 23,2024 jijini Dodoma.
Mwenyekiti wa Bodi ya Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) Dk.Fatma Kassim Mohammed,akielezea lengo la baraza hilo wakati wa uzinduzi wa Baraza la Wafanyakazi la Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) lililofanyika leo Oktoba 23,2024 jijini Dodoma.
MWAKILISHI wa Mjumbe wa Baraza Kuu Serikalini Bi.Maisha Mbilla,akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Wafanyakazi la Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) lililofanyika leo Oktoba 23,2024 jijini Dodoma.
SEHEMU ya washiriki wakimsikiliza Naibu Waziri wa Ujenzi Mhandisi Godfrey Kasekenya (hayupo pichani) wakati akizindua Baraza la Wafanyakazi la Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) lililofanyika leo Oktoba 23,2024 jijini Dodoma.
SEHEMU ya washiriki wakimsikiliza Naibu Waziri wa Ujenzi Mhandisi Godfrey Kasekenya (hayupo pichani) wakati akizindua Baraza la Wafanyakazi la Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) lililofanyika leo Oktoba 23,2024 jijini Dodoma.
NAIBU Waziri wa Ujenzi Mhandisi Godfrey Kasekenya,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuzindua Baraza la Wafanyakazi la Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) lililofanyika leo Oktoba 23,2024 jijini Dodoma.


Na Okuly Julius -DODOMA


NAIBU Waziri wa Ujenzi Mhandisi Godfrey Kasekenya,amesema Baraza la Wafanyakazi la NCC ni jukwaa muhimu mahala pa kazi linalotumika kama kiunganishi kati ya Menejimenti na Wafanyakazi.

Mhandisi Kasekenya ameyasema hayo leo Oktoba 23,2024 jijini Dodoma wakati akizindua Baraza la Wafanyakazi la Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC).

Amesema kupitia baraza la wafanyakazi na Menejimenti wanapata fursa ya kujadili kwa pamoja masuala ya msingi ya taasisi ikiwemo mipango, Bajeti na masuala mengine ya kiutendaji na kiutawala ili kuweza kufikia malengo na matarajio ya Watumishi wa Taasisi.

“Baraza la Wafanyakazi ni jukwaa muhimu sana mahala pa kazi linalotumika kama kiunganishi kati ya Menejimenti na Wafanyakazi,”amesema

Ameongeza kuwa :”Kupitia Baraza hili, Wafanyakazi na Menejimenti mnapata fursa ya kujadili kwa pamoja masuala ya msingi ya Taasisi ikiwemo mipango, Bajeti na masuala mengine ya kiutendaji na kiutawala ili kuweza kufikia malengo na matarajio ya Watumishi wa Taasisi,”.

Hata hivyo Mhandisi Kasekenya amesema kuwa maeneo ambayo mabalaza yanafanya kazi ipasavyo migogoro kati ya Menejimenti na Watumishi haiwezi kutokea.

Kwa upande wake Mwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya UjenziBw. Mrisho Mrisho amesema baraza la wafanyakazi ni muhimu kwasababu ni kiunganishi muhimu na husaidia kuboresha mahusiano baina ya wafanyakazi mahala pa kazi.

“Balaza la wafanyakazi ni chombo muhimu kwa maslahi ya taasisi na taifa kwa ujumla,”amesema

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Baraza la NCC Dk.Fatma Kassim Mohammed ametaja kazi ya baraza hilo kuwa ni kushauri menejimenti na kuimarisha uhusiano mahala pa kazi.

Amesema baraza la wafanyakazi ni muhimu mahala pa kazi kwasababu husaidi kuboresha utendaji kazi wa taasisi wa maslahi ya taifa.

“Baraza la wafanyakazi ni muhimu kwasababu ni kiunganishi muhimu kati ya menejimenti na wafanyakazi na husaidia katika kuimarisha mahusiano ya taasisi na kuleta tija katika utendaji kazi,”amesema

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post