TANZANIA KUWA KITOVU CHA KIMATAIFA CHA UBUNIFU WA TEKNOLOJIA NA BAHARINI

Ushirikiano  kati ya Taasisi ya Adani Foundation na IITM Zanzibar kwa pamoja wamekubaliana  katika kuboresha elimu ya juu nchini katika kuunda fursa kwa vijana, hasa wale wanaotoka katika familia zenye hali duni.

Kwa kuanzisha programu wezeshi  ya Sayansi ya Takwimu, Akili Bandia, na Miundo ya Baharini, huu ni mpango unaokamilisha malengo makubwa ya serikali ya kujenga uchumi unaoendeshwa na maarifa, na kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha kimataifa cha ubunifu wa teknolojia na baharini. 

Ushirikiano huu hautawainua tu wanafunzi wa Kitanzania bali pia utachangia ajenda ya maendeleo ya muda mrefu ya taifa kwa kuwapa viongozi wa baadaye ujuzi unaohitajika katika sekta muhimu.

Ni maono ya serikali ya Tanzania juu ya Elimu kuwa  msingi wa maendeleo ya kitaifa yamepata  mshirika katika Taasisi ya Adani Foundation, ambayo ina historia ndefu ya kuziwezesha  jamii kupitia elimu na maendeleo endelevu. 

Msisitizo wa serikali wa kuhakikisha mipango kama hii inafanikiwa unaonyesha uwekezaji wake endelevu katika watu wake na mustakabali wa taifa.

Tanzania inaendelea kusonga mbele katika kutimiza malengo yake ya kimkakati ya maendeleo endelevu, ukuaji wa uchumi, na kuwawezesha vijana, ikiwa na msingi thabiti wa imani kwamba elimu ni ufunguo wa kufungua uwezo wa taifa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post