DUWASA YAPONGEZWA JITIHADA ZA HUDUMA YA MAJI DODOMA

 


Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imeipongeza Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA) kwa jitihada inazochukua za muda mfupi za uchimbaji visima maeneo ya pembezoni mwa Jiji la Dodoma kuhakikisha wananchi waliyopo katika maeneo ya pembezoni wanapata huduma ya maji.

Pongezi hizo zimetolewa leo Oktoba 09, 2024 wakati wa Kikao cha Kamati ya PAC kilichoongozwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Naghenjwa Kaboyoka.

Aidha, Kamati hiyo imeiagiza DUWASA kufanyia kazi kwa wakati Hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).





Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post