KAMATI YA BUNGE YAMPONGEZA RAIS DKT SAMIA SULUHU KWA KUCHOCHEA MAZINGIRA MAZURI YA UWEKEZAJI NCHINI

 

 Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt.Suleiman Jafo akizungumza wakati wa ziara ya  ya siku moja ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Uwekezaji na Biashara ilipotembelea eneo Kituo cha Forodha za Tanzania na Kenya eneo la Mkinga Mkoani Tanga kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mariam Ditopile Mzuzuri akifuatia Mkuu wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian
 Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mariam Ditopile Mzuzuri akisisitiza jambo wakati wa ziara hiyo



Na Oscar Assenga, MKINGA

 

KAMATI ya Kudumu ya Bunge Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imempongeza Rais Dkt Samia Suluhu kwa kazi kubwa anayoifanya kuchochea uwekezaji nchini pamoja na kuweka mazingira mazuri kwa wafanyabiashara.

Pongezi hizo zilitolewa leo na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo Mariam Ditopile Mzuzuri wakati wa ziara ya siku moja ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Uwekezaji na Biashara ilipotembelea eneo Kituo cha Forodha za Tanzania na Kenya eneo la Mkinga Mkoani Tanga.

 

Alisema kwamba mazingira hayo mazuri yamewekwa kwa wafanyabiashara ambao tayari wapo kwenye biashara na viwanda ambavyo vinazalisha bidhaa mbalimbal nchini

 

“Leo tumepata fursa ya kuja hapa kituo cha Forodha Horohoro kuona namna kituo hicho cha pamoja baina ya Tanzania na Kenya sisi kama kamati tunawapongeza kwani kituo hiki kazi yake kubwa kukusanya mapato kuhakikisha wafanyabishawa kutoa Kenya wanaoleta bidhaa hawapitia njia za panya wanapitia hapo kutoa ushuru na kodi stahiki pia bidhaa zinazotoka nchini na kwenda nchi jirani zinatoa ushuru stahiki “Alisema

 

Alisema wanawapongeza kuongeza ukusanyaji wa mapato kwenye kituo hicho kwa maana mwaka jana walipanga kukusanya jumla ya sh.Bilioni 77 lakini walikusanya Bilioni 90 na kwa mwaka huu wa fedha wa 2024/2025 kota ya kwanza Julai hadi Sept walipangiwa kukusanya Bilioni 25 lakini wamekusanya bilioni 34 wanaona ni mafanikio.

 

“Sisi kama Kamati tunaiomba serukali na tutalisimamia lazima waongeze ufanisi katika kituo hicho na kikubwa cha kwanza ambacho kimeelezwa ni ununuzi wa scana kwa namna tulivyoona ukusanyaji wa mapato unaridhisha lazima tupate scana na focklift kwa ajili ya kunyanyua mizigo tuweze kuongeza ufanisi na mapat kupanda”Alisema

 

Aidha alisema kwamba inawezekana wanaotumia njia za panya ni kutokana na kukaa muda mrefu wakati wa kupitisha mzigo na hivyo kuona shida kupitishia hapa hivyo tunaiagiza Serikali ndani ya muda mfupi na wizara zote husika na Waziri Dkt Jafo akae na Waziri wa Fedha ili kwa haraka scana na focklift ziweze kupatikana na kuongeza ufanisi na kituo kifanye kazi ile inayokusudiwa chini ya uongozi wa Rais Dkt Samia Suluhu na Serikali yake ya wamu ya sita.

 

Awali akizungumza wakati wa ziara hiyo Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt.Suleiman Jafo amesema kwamba Serikali itahakikisha bidhaa zote zinazopitishwa kwenye vituo vya Forodha katika mipaka ya Tanzania na nchi jirani zinaendelea kuwa na viwango vinavyokidhi na kudhibitishwa na Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Wakala wa VipimoTanzania ( WMA) na Tume ya Ushindani (FCC).

 

Alisema kwamba lengo la kuhakikisha hilo ni kuwalinda watanzania na walaji wa mwisho wa siku wafanye biashara na kamati imetoa maelekezo kuhakikisha eneo hilo linakuwa na scana ambayo inaweza kuhakikisha mizigo inakwenda kwa haraka sana.

 

“Hili la scana hapa tumelichukua na sio muda mrefu kupitia Wizara ya fedha tutahakikisha Scana hiyo inapatikana pamoja nyenzo za kufanyia kazi ikiwemo Focklift itakayokuwa ikinyanyua mizigo lakini niwashukuru Kamati ya Bunge kwa kazi kubwa na niwaambie serikali itahakikisha mambo yote muhimu yanatekelezwa lengo kubwa ni kuboresha utoaji huduma”Alisema Waziri Jafo.

 

 Aidha alimshukuru R ais Dkt Samia Suluhu kutokana na kazi kubwa inayoendelea katika maeneo mbalimbali ya kimaendeleo na hata kamati ilivyotembelea eneo la Horohoro imeona kuna mafanikio makubwa kwenye ongezeko la mapato.

 

“Lakini kuona jinsi gani Taasisi zinasaidia kuhakikisha biashara eneo hilo mizigo isafirishwe vizuri baina ya nchi ya jirani kenya na bidhaa zinazopita lazima zinakidhi viwango vilivyowekwa na kuthibitishwa na TBS na WMAna FCC lengo kuwalinda watanzania na walaji mwisho”Alisema Waziri Dkt Jafo.

 

Akizungumzia suala la ubinafsishaji lililofanyika miaka ya nyuma nchini alisema Serikali ilikuwa na nia njema kufanya ubinafsishaji lakini kwa bahati mbaya malengo yalienda tofauti wengi waliopewa viwanda hawakufanya vizuri.

 

“Kama mnakumbuka hivi karibuni Rais Dkt Samia Suluhu alitoa maelekezo kwamba viwanda hivyo vifufuliwe maeneo mbalimbali na nilikuja Tanga na hivi karibuni tumekaa kikao na Hazina kubainisha viwanda vyote na kuona hatua za kuchukua“Alisema

 

Waziri Dkt Jafo alisema mojawapo ya hatua hizo ni kuhakikisha viwanda ambavyo vilikuwa havifanyi kazi waangalia namna bora ya kufanya kazi kwa utaratibu wa kisheria na wapate wawekezaji wengine au waliokuwepo wahakikishe ndani ya muda mfupi wanafanya uwekezaji ili viwanda viweze kufanya kazi na kutengeneza ajira kwa watanzania.

 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post