MAFIA BOXING PROMOTION WAUNGA MKONO KAMPENI YA RAIS DKT SAMIA SULUHU YA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

 




Na Oscar Assenga,TANGA

KAMPUNI ya Mafia Promotion Boxing imetoa msaada wa majiko ya Gesi kwa wanawake wanaojishughuli na uuzaji wa vyakula katika masoko ya Mgandini, Makorora na Mlango wa Chuma yaliyoko jijini Tanga ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Rais Dkt Samia Suluhu ya matumizi ya Nishati Safi ya kupikia.

Licha ya kugawa mitungi hiyo ya gesi lakini wametoa msaada mwengine wa vitu mbalimbali katika kituo cha kulea watoto yatimacha Green Cresent Ophanege Foundation cha Jijini humo .

Hatua ya kampuni hiyo kuunga mkono juhudi hizo inatokana na ushindi walioupata mabondia mbalimbali wanaodhaminiwa na kampuni hiyo ambao walipata ushindi katika mapambano yao walipopanda hivi mwanzoni mwa mwezi 0ctoba mwaka huu Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza Mkurugenzi wa Matangazo na Uzalishaji kutoka Kampuni ya Mafia Promotion Omari Clayton alisema pambano hilo lilichagizwa na Technical Knock Out ‘KO’ ya Rais Dkt. Samia Suluhu.

Alisema baada ya ushindi huo wapewa fedha taslimu kama zawadi kwa mabondia hao ambayo imewatia hamasa kuhakikisha wanazidi kuijengea heshima Tanzania kupitia mchezo wa ngumi.

Alisema kwamba jambo ambalo wameifanya kwa kugawa majiko hayo ya gesi ni kama sehemu ya kurudisha kwa jamii ikiwa ni utaraibu wao na wanaungana na watanzania kupitia Kampeni ya Rais Dkt. Samia ya kuhamasisha juu ya matumizi ya nishati safi na kuachana na matumizi ya mkaa na kuni katika kupikia na shughuli nyingine hali ambayo inasababisha mabadiliko ya tabianchi na uzalishaji wa hewa ukaa.
Alisema kwamba kampuni hiyo ya Mafia wanaunga mkono juhudi za Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika kupambana na kuhamasisha watanzania kuhama kutoka kwenye matumizi ya mkaa na kuni kupikia na kwenda kwenye matumizi ya nishati safi.

“ Ndio maana leo tumegawa majiko ya gesi kwa mama zetu wanapika vyakula katika masoko yaliyopo katika jiji la Tanga” Alisema Clayton.
“Tumehamasika na tunampongeza sana Rais wetu Dkt. Samia kuja na ‘KO ya Mama’ na kuwazawadia mabodia wetu ambao walipambana kuhakikisha wanabakisha mikanda hapa Tanzania na walifanikiwa na tunamuahidi kwamba mama kupitia Mafia Boxing tutazidi kuiheshimisha Tanzania”Alisema .

Akizungumza kwa niaba ya mabondi wenzanke Ibrahim Mafia alisema kwamba haikuwa rahisi kupamba ulingoni kutokana na mpinzani wake kuwa imara lakini kupitia maombi ya watanzania alipambana kuhakikisha anawapa furaha kwa kupata ushindi .

“Ule ushindi ni ushindi ni ushindi wetu lakini pia ni ushindi wa watanzania walikuwa wakituombea tumepokea zawadi kutoka kwa Rais wetu mama Samia tukaona hatuwezi kuitumia peke yetu bali tushirikiane kile ambacho tumepata kwa kuwapa majiko ya gesi na kutoa msaada kwa kituo cha watoto yatima tunaomba mzidi kutuombea dua ili wakati mwingine tuweze kutoa kikubwa zaidi. Alisema Mafia”

Bondia Ibrahim Mafia alipanda ulingoni kuzichapa na mpinzani wake Enoch Tettey raia wa Ghana kuwania mkanda wa dunia ‘World Boxing Council Bantamweight’ wenye uzito wa Kg 53 katika ukumbi wa City Center Hall Magomeni Sokoni na hatimaye kufanikiwa kubwaga chini mpinzani wake kwa KO.
Hata hivyo wakina mama mntilie ambao walipata majiko hayo waliwapongeza mabondia wote kwa ushindi walioupata pamoja na kuishukuru Kampuni ya Mafia Boxing Promotion kwa kuwapatia mitungi ya gesi ambayo itawasaidia katika shughuli zao.
Tunawashukuru kwa zawadi zenu na sisi tunaendelea kuwaombea kwa Mungu hakika atawalipa tulikuwa na changamoto ya kupata mkaa kwa ajili ya kupikia lakini sasa kupitia majiko haya yatatusaidia kurahisisha shughuli zetu za kupika kila siku .

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post