MAFUNZO YA BARAZA LA WAFANYAKAZI WA OWMS

Naibu Wakili Mkuu wa Serikali Bi.Alice Mtulo, akizungumza na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali, wakati akifunga Mafunzo kuhusu Udhibiti Msongo wa Mawazo, Maandalizi ya Kustaafu katika utumishi na Uongozi na Dhana ya Ujumuishi wa Anuai za Kijamii yaliyofanyika mkoani Dodoma.
Naibu Wakili Mkuu wa Serikali Bi. Alice Mtulo (aliyesisima kulia) akipokea zawadi ya kitabu cha kujiandaa kustaafu utumishi wa umma kutoka kwa mtoa mada Dkt. Venance Shilingi mara baada ya kutoa mada kuhusu Maandalizi ya Kustaafu katika Utumishi na Uongozi kwenye mafunzo ya Baraza la Wafanyakazi yaliyofanyika mkoani Dodoma.
Dkt. Venence Shilingi akitoa mada kuhusu Maandalizi ya Kustaafu katika Utumishi na Uongozi kwenye mafunzo ya Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali yaliyofanyika mkoani Dodoma.
Bi. Mwanaamani Mtoo akitoa mada kwa wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali kuhusu Dhana ya Ujumuishi wa Anuai za Kijamii wakati mafunzo hayo yaliyofanyika mkoani Dodoma.

Bi. Bupe Kalonge akitoa mada kwa wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali kuhusu Udhibiti wa Msongo wa Mawazo wakati wa mafunzo hayo yaliyofanyika mkoani Dodoma.

Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wakimsikiliza Naibu Wakili Mkuu wa Serikali Bi. Alice Mtulo wakati akifunga mafunzo kuhusu Udhibiti Msongo wa Mawazo, Maandalizi ya Kustaafu katika utumishi na Uongozi na Dhana ya Ujumuishi wa Anuai za Kijamii yaliyofanyika mkoani Dodoma.

Afisa TEHAMA wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali Bw. Nyamhoni Chacha akichangia mada kuhusu Msongo wa Mawazo wakati wa mafunzo kuhusu Udhibiti Msongo wa Mawazo, Maandalizi ya Kustaafu katika utumishi na Uongozi na Dhana ya Ujumuishi wa Anuai za Kijamii yaliyofanyika mkoani Dodoma.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post