MBUNGE UMMY APITA VIJIWENI KUHIMIZA WANANCHI KUJIANDIKISHA NA KUSHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA.

 


Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini (CCM) Mhe Ummy Mwalimu leo tarehe 18/10/2024 ametembelea vijiwe mbalimbali katika mitaa ya Mwambani, Mchukuuni, Mwahako, Mwakidila na Mwang'ombe katika kata za Tangasisi na Masiwani kuhamasisha wananchi kujiandikisha katika daftari la mkazi na pia kushiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakao fanyika tarehe 27/11/2024.


Mhe Ummy ameeleza kuwa Mitaa ndio chimbuko la Amani na Maendeleo kwa Wananchi hivyo ni muhimu kila mwananchi wa Tanga Mjini kushiriki.





Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post