MBUNGE UMMY-KAZI YA MAENDELEO ILIYOFANYWA NA RAIS DKT SAMIA SULUHU MKOANI TANGA SIO YA KUTAFUTA KWA TOCHI




Na Oscar Assenga,TANGA

MBUNGE wa Jimbo la Tanga Ummy Mwalimu amesema kazi ya Rais Dkt Samia Suluhu anayoifanya ya Maendeleo katika Mkoa wa Tanga sio ya kutafuta kwa Tochi.

Ummy aliyasema hayo leo wakati akitoa salamu katika Kongamano la Samia Challenge 2024 ambalo limeandaliwa na African Anti-Violence Journalist lililofanyika Jijini Tanga kwenye ukumbi wa Samia Business Centre Kange.
Ambapo alisema  kuna miradi mingi ya maendeleo ikiwemo ya Afya,Umeme,Elimu,Maji na Vitega Uchumi karibia kila kona ambayo imechangia kuinua uchumi wa mkoa wa Tanga.

Alisema kwa sababu katika kila eneo la maendeleo utamkuta Rais Samia na kubwa zaidi ambalo wanajivunia nalo ni maboresho makubwa ya Bandari ya Tanga ambapo uwekezaji uliofanywa na Rais Dkt Samia Suluhu ni wa Bilioni 429.1

“Kutokana na hili sasa tunatembelea kifuata mbele kutokana na uwekezaji huo ambao umeufanya mkoa huo kuanza kupokea meli kubwa zinazoleta shehena za magari na hilo linaonyesha matunda ya uwekezaji katika Bandari kwa kuchimbwa kina na meli kutia nanga gatini “Alisema

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post