MKATABA WA BILIONI 13.5 WASAINIWA KWA UJENZI WA JENGO LA TIA SINGIDA

Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo (kulia) pamoja na Mwakilishi wa Salem Construction, Charles Casmir (kushoto) wakionesha mkataba waliosaini kwaajili ya ujenzi wa jengo la TIA kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.

************************

TAASISI ya Uhasibu Tanzania (TIA), imesaini mkataba na kampuni ya Salem Construction kwaajili ujenzi wa jengo la kampasi yake mkoani Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5.

Mkataba huo utachukua miezi 24 hadi kukamilika kwa ujenzi jengo hilo mkoani Singida.

Akizungumza leo Oktoba 15,2024 katika hafla hiyo iliyofanyika kwenye ofisi za taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam, Mtendaji Mkuu wa TIA, Prof. William Pallangyo amesema fedha za ujenzi wa kampasi hiyo zimetolewa chini ya Mradi wa Mageuzi ya Kiuchumi kwa Vyuo Vikuu nchini (HEET) unaofadhiliwa na Benki ya Dunia (WB).

Aidha amemtaka mkandarasi kuhakikisha anajenga jengo lenye ubora na kufanyakazi kwa karibu na wananchi wa Singida ili wawe walinzi wa mradi huo mpaka utakapokamilika kwa muda ambao umewekwa.

“Tumemtaka mkandarasi azingatie kanuni za ujenzi ili kuhakikisha wafanyakazi wanakuwa salama wakati wote tunataka mpaka mradi unapokamilika watu wawe salama kusitokee kifo hata kimoja wala majeruhi,” amesema Prof. Pallangyo.

Amesema watajitahidi kufanyakazi kwa karibu na benki ya dunia ambayo ndiyo inayofadhili mradi huo kuhakikisha kila mkandarasi anapoomba malipo analipwa kwa wakati ili mradi usisimame.

Kwa upande wake Mratibu wa HEET Kitaifa, Dkt. Kenedy Hossea, ameipongeza TIA na menejimenti yake kwa kupata mkandarasi mapema kwaajili ya ujenzi wa jengo katika Kampasi ya Singida

“Nawapongeza Mtendaji Mkuu wa TIA kwasababu kuna watu walianza muda mrefu hawajapata mkandarasi mpaka sasa wanalumbana tu zabuni inatangazwa inafutwa wanashindwa kufikia muafaka,” amesema

Pamoja na hayo, Dkt. Hossea amemtaka mkandarasi wa jengo hilo kuzingatia ubora na kuahidi kuwa wataalamu wanaosimamia mradi huo kutoka wizarani watakuwa wakipita mara kwa mara kuhakikisha ubora unazingatiwa.

Nae Mwakilishi wa Salem Construction, Charles Casmir, amesema mkataba huo ni wa miezi 24 lakini kwa namna walivyojipanga watakamilisha mradi huo ndani ya miezi 18.

Amesema wanatarajia kuwa jengo hilo litakuwa la mfano na kwamba watahakikisha wanazingatia usalama wa wafanyakazi na jamii inayozunguka mradi huo katika Mkoa wa Singida.

Mratibu wa mradi wa huo TIA , Oyombe Simba, aliishukuru serikali kwa kukubali fedha hizo kupelekwa kwenye taasisi hiyo kwaajili ya kuboresha mazingira ya wanafunzi kujisomea.

Amesema TIA imepokea jumla ya shilingi bilioni 27.6 ambazo zinakwenda kuboresha kampasi za taasisi hiyo ambapo mbali na ujenzi wa jengo la Singida pia watajenga majengo kwenye kampasi ya Mwanza.

Hata hivyo amesema jengo la bweni litakalojengwa Mwanza litagharimu shilingi bilioni 7.2 na litakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi 306 kwa wakati mmoja.

“Mbali na ujenzi wa majengo mradi huu umelenga kuboresha mitaala na kuwajengea uwezo wakufunzi kwenye taasisi yetu kwa hiyo tunapoanza kutekeleza mradi huu ni fahari kubwa sana kwetu,” amesema
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo (kulia) pamoja na Mwakilishi wa Salem Construction, Charles Casmir (kushoto) wakisaini mkataba wa ujenzi wa jengo la TIA kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo (kulia) pamoja na Mwakilishi wa Salem Construction, Charles Casmir (kushoto) wakisaini mkataba wa ujenzi wa jengo la TIA kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo (kulia) pamoja na Mwakilishi wa Salem Construction, Charles Casmir (kushoto) wakisaini mkataba wa ujenzi wa jengo la TIA kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo (kulia) pamoja na Mwakilishi wa Salem Construction, Charles Casmir (kushoto) wakionesha mkataba waliosaini kwaajili ya ujenzi wa jengo la TIA kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo (kulia) pamoja na Mwakilishi wa Salem Construction, Charles Casmir (kushoto) wakipongezana huku wakionesha mkataba waliosaini kwaajili ya ujenzi wa jengo la TIA kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo (kulia) pamoja na Mwakilishi wa Salem Construction, Charles Casmir (kushoto) wakipongezana huku wakionesha mkataba waliosaini kwaajili ya ujenzi wa jengo la TIA kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo (kulia) pamoja na Mwakilishi wa Salem Construction, Charles Casmir (kushoto) wakionesha mkataba waliosaini kwaajili ya ujenzi wa jengo la TIA kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mratibu wa HEET Kitaifa, Dkt. Kenedy Hossea akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa jengo la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mratibu wa HEET Kitaifa, Dkt. Kenedy Hossea akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa jengo la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mratibu wa HEET Kitaifa, Dkt. Kenedy Hossea akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa jengo la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa jengo la TIA kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa jengo la TIA kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa jengo la TIA kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Makamu Mkuu wa Chuo- Taaluma, Utafiti na Ushauri wa kitaalamu TIA, Dkt. Momole Kasambala akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa jengo la TIA kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Watumishi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) wakiwa katika hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa  jengo la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Watumishi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) wakiwa katika hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa  jengo la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Watumishi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) wakiwa katika hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa  jengo la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Watumishi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) wakiwa katika hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa  jengo la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Watumishi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) wakiwa katika hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa  jengo la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Watumishi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) wakiwa katika hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa  jengo la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo, Mratibu wa HEET Kitaifa, Dkt. Kenedy Hossea, Mratibu wa mradi wa HEET katika taasisi ya (TIA), Oyombe Simba pamoja na wadau wengine wakiwa kwenye picha ya pamoja katika hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa  jengo la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post