NLD YAZOA WANACHAMA KUTOKA VYAMA VYA ACT WAZALENDO, ADC

 

Na Oscar Assenga, TANGA


ZAIDI ya Wanachama 150 kutoka vyama vya ADC na ACT wazalendo wamejiunga na Chama cha NLD  Mariam Sijaona aliyekuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ACT Wazalendo na Scola Kahana aliyekuwa mgombea wa nafasi ya makamo mwenyekiti bara kupitia ADC na mgombea ubunge Jimbo la kibaha katika uchaguzi wa 2020.

Idadi hiyo kubwa kujiunga na chama hicho inaonyesha namna wanavyokubalika kutokana na sera zao na hivyo kuendelea kuwaimarisha kuelekea kwenye chaguzi mbalimbali ikiwemo Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na ule mkuu wa mwaka 2025

Akizungumza wakati akiwapokea wanachama hao wapya Katibu Mkuu wa Chama hicho Doyo Hassan Doyo alisema kwamba kupokelewa kwa idadi hiyo ya wanachama kunaashiria mwelekeo mzuri wa chama hicho ambacho kwa sasa wanatarajia kuanza ziara za kujitambulisha kwa wanachama na kutangaza sera zao nchi nzima .

Aidha alisema ziara hiyo itaanza  Oktoba 30 mwaka huu  ikianzia mkoani Tanga, Pemba,Kanda ya Ziwa na Mikoa ya Kanda ya Kaskazini ambapo watakuwa na mikutano katika maeneo mbalimbali

Doyo, alisema katika zoezi hilo la kupokea wanachama hao wapya wakiwemo  viongozi wengine wa NLD, akiwemo Makamo Mwenyekiti Bara,Khamis Said Hamad ambapo waliwakaribisha wanachama hao wapya na kuwahakikishia kuwa wana haki sawa na wanachama wa chama hicho kwa mujibu wa katiba ya NLD.

Alisema kwamba wanachama hao wameamua kujiunga na Chama cha NLD kwa sababu ni haki yao ya kikatiba na ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Doyo katika kukuza Demokrasia nchini.

"Tunajua chama chetu kipya hakina ruzuku, lakini tupo tayari kukaa na njaa ili kupigania demokrasia ya kweli na hatimaye chama chetu kufanya vizuri kwenye chaguzi zijazo," walisisitiza wana chama hao.

Doyo aliwasihi wanachama hao wapya kusoma Itikadi ya NLD, akisisitiza kuwa Itikadi ya chama hicho imebeba uzalendo, haki, na maendeleo.


Katika hatua nyengine Chama cha National League for Democracy (NLD) kimewasilisha ombi kwa serikali kuhusu kalenda ya uchaguzi iliyotolewa na Tamisemi ambapo wameiomba  Serikali kuketi na wadau wa Uchaguzi hususani vyama vya Siasa kuona namna wanavyoweza kuongeza muda wa kampeni.

 Doyo alisema  muda uliotolewa kwa maandalizi ya uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji, na vitongoji ni mfupi sana na kwamba hautoshi.

Alisema kutokana na hilo ni vyema uchaguzi huo  ukasogezwa mbele ili kuongeza muda wa kampeni  ili kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa haki na ufanisi bila vikwazo,

"Kupewa siku saba hadi siku kumi na nne, siku hizo haziwezi kutosha,wagombea wanahitaji muda mrefu wa kampeni Lakini pia Wananchi wanahitaji muda mrefu wa kuwachuja wagombea wao,hivyo Tunaiomba serikali kupitia Tamisemi isogeze mbele muda wa Uchaguzi, sio kuahirisha uchaguzi, bali kuongeza muda wa maandalizi,"Alisisitiza Doyo

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post