SMAUJATA TANGA YAWATAKA VIJANA KUCHAGUA VIONGOZI WATAKAOKUWA SAUTI YA WANANACHI





Na Oscar Assenga, TANGA

VIJANA Mkoani Tanga wametakiwa kuhakikisha wanawachagua viongozi ambao watakuwa sauti ya wananchi kwenye maeneo yao na sio wachuma tumbo wakati wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 27 mwaka huu .

Wito huo ulitolewa leo na Mkuu wa Idara ya Vijana Hamasa Smaujata Mkoa wa Tanga Athumani Sheria wakati akizungumza na mtandao huu ambapo alisema vijana ni muhimu kuhakikisha wanashiriki kwenye uchaguzi huo kwa wingi ili waweze kuwachagua viongozi ambao watawapa maendeleo.

Alisema kwa sababu lazima viongozi wanaowachagua wawe ambao wanajitokeza na kuwa mstari wa mbele katika kusimamia maendeleo katika maeneo yao kwa kushirikiana na wananchi.

“Ndugu zangu vijana katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa tuhakikishe tunatumia haki yetu ya msingi kuwachagua viongozi ambao watakuwa sauti ya wananchi kwa kuchochea maendeleo na sio wachuma tumbo”Alisema Sheria

Hata hivyo aliwataka vijana kuhakikisha wanajitokeza kuwania nafasi mbalimbali za uongozi kwenye uchaguzi huo kutokana na kwamba mchango wao kwenye maeneo yao unaweza kuwa na tija kubwa katika kusukuma gurudumu la maendeleo

Aidha pia alisema kwamba wanamshukuru Rais Dkt Samia Suluhu kwa uwekezaji wa Bilioni 429.1 katika Bandari ya Tanga ambayo yamewezesha maboresho makubwa na hivyo kuufungua kiuchumi mkoa huo.

Alisema maboresho hayo yamewasaidia kupata ajira lakini Serikali kuongeza pato pamoja na kuwainua kiuchumi vijana wa bodaboda na mama lishe ikiwemo wafanyabiashara mbalimbali mkoani humo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post