TAIFA STARS YACHAPWA 2-0 NA CONGO DRC


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

TIMU ya Taifa ya Tanzania imeshindwa kutamba katika dimba lake la nyumbani mara baada ya kupokea kichapo cha mabao 2-0 dhidi ya timu ya Taifa ya Congo DR.

Katika mchezo huo wa kufuzu AFCON 2025 ulipigwa kwenye dimba la Benjamini Mkapa Jijini Dar es Salaam, timu zote zilicheza soka safi, licha ya Congo DR kutengeneza nafasi nyingi za mabao bila mafanikio kwenye kipindi cha kwanza.

Mpaka mapumziko mechi ilikuwa 0-0, hadi kipindi cha pili timu zote ziliweza kufanya mabadiliko kwa baadhi ya wachezaji ili kuweza kupata matokeo, lakini bahati ilikuwa kwa Congo DR ambao walimtoa Silas na nafsi yake kuchukuliwa na Meschack Elia ambaye aliweza kupachika mabao mawili ambayo yaliiwezesha Congo DR kuondoka na ushindi kwenye mchezo huo.

Congo DR iliweza kupata mabao kupitia kwa Elia dakika ya 88 ya mchezo pamoja na dakika nne za nyongeza na matokeo kuwa 2-0.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post