
Mjumbe wa kamati tendaji ya Mwanza Press Club Tonny Alphonce

Akichangia mada ya kanuni za uchaguzi na nafasi ya vyombo vya habari katika uchaguzi ujao kwenye mkutano wa MISA - TAN na Wadau, Mjumbe wa kamati tendaji ya Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Mwanza (Mwanza Press Club) Tonny Alphonce amesema kuna umuhimu wa taasisi zingine kutoa elimu ya uchaguzi mkuu kama walivyofanya TAKUKURU mkoa wa Mwanza.
Alphonce amesema kipindi cha uchaguzi kinagusa jamii nzima hivyo taasisi zote zinazofanya kazi na wananchi zina wajibu wa kutoa elimu ya uraia ili makundi yote yaweze kushiriki kwa manufaa ya taifa.
"Watoa mada wamesema hapa uchaguzi ni mchakato,Mimi niwapongeze TAKUKURU mkoa wa Mwanza ninapotoka kwa kuwa wao walitoa elimu na kusisitiza kuwa kuna umuhimu wa kuripoti habari kabla,wakati na baada ya uchaguzi", amesema Alphonce.
Hayo yamejadiwa katika Mkutano ulioandaliwa Taasisi ya vyombo vya habari kusini mwa Afrika tawi la Tanzania(Misa Tan) Kwa kuwakutanisha Wadau mbalimbali kuangalia ushirikiano wa pamoja.
Social Plugin