Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

MWANAMKE MWENYE UALBINO AKUTWA AMEFARIKI NDANI MLANGO UKIWA UMEFUNGWA NJE




Mwanamke mwenye ualbino aliyefahamika kwa jina la Wande Mbiti (38)  amekutwa amefariki dunia nyumbani kwake alipokuwa akiishi maeneo ya Nhelegani kata ya Kizumbi manispaa ya Shinyanga huku mlango wa nyumba yake ukiwa umefungwa kwa kufuli kwa nje.

Tukio hilo limetokea Machi 02, 2025 katika Kijiji cha Nhelegani kata ya Kizumbi manispaa ya Shinyanga Mkoani Shinyanga.

Inaelezwa kuwa majira ya mchana majirani zake Wande Mbiti walisikia harufu kali wakati wakichuma mboga katika moja ya shamba lililopo jirani na nyumba yake iliyokuwa imefungwa kwa nje ndipo waliita viongozi wa kijiji na mtaa na kulitaarifu jeshi la polisi lililofika na kuvuja mlango na kukuta maiti ya Wande Mbiti ikiwa kitandani.

Mwenyekiti wa Chama cha watu wenye ualbino Mkoa wa Shinyanga Yunis Manumbu amesema amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Wande Mbiti na kulaani vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa watu wenye ualbino kwenye familia na jamii kwa ujumla huku Mtendaji wa kata ya Kizumbi Livingston Alea akitoa rai kwa jamii.

Kaimu Kamanda wa Jeshi la polisi Mkoani Shinyanga ACP. Kennedy Mgani amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi kubaini sababu ya kifo chake.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com