Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

CCM YAZINDUA WIKI YA WAZAZI MKOANI SHINYANGA | MLOLWA: “WAZAZI NI NGUZO YA MAENDELEO NA MAADILI”


Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mabala Mlolwa, akizungumza kwenye uzinduzi wa wiki ya Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga leo Aprili 9, 2025.

Na Sumai Salum - Kishapu

Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga kupitia Jumuiya ya Wazazi,  kimezindua rasmi Wiki ya Wazazi kwa kufanya shughuli mbalimbali za kijamii katika Wilaya ya Kishapu, ikiwemo ukaguzi wa miradi ya maendeleo, upandaji miti na mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari Bunambiyu.

Uzinduzi huo umefanyika leo Aprili 9, 2025, ukihudhuriwa na viongozi wa chama, jumuiya zake, wanachama pamoja na wananchi, ambapo Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mabala Mlolwa, alikuwa mgeni rasmi.

Akizungumza katika mkutano huo wa hadhara, Mhe. Mlolwa amewahimiza wazazi kushiriki kikamilifu katika malezi bora ya watoto na kusimamia maadili ya jamii, akieleza kuwa wazazi ni nguzo muhimu ya kuimarisha msingi wa taifa.

“Jumuiya ya Wazazi CCM imeendelea kuwa chombo madhubuti ndani ya CCM, si tu kwa ajili ya ushauri bali pia kwa kusimamia maadili, kukemea maovu na kuhamasisha maendeleo ya jamii,” amesema Mhe. Mlolwa.

Aidha, ametumia jukwaa hilo kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo inayogusa sekta mbalimbali mkoani Shinyanga, ikiwemo elimu, afya na miundombinu.

Katika ziara hiyo, Mlolwa ametembelea na kukagua miradi ya maendeleo katika shule ya sekondari Bunambiyu ambapo Mkuu wa shule hiyo, Mzee Matata Joel, ameeleza kuwa zaidi ya shilingi milioni 166.4 zimetolewa na serikali ndani ya miaka mitano, fedha ambazo zimetumika kujenga madarasa, ofisi za walimu na matundu ya vyoo.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Shinyanga, John Siagi, amesema kuwa wameandaa mpango kazi kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025 kwa lengo la kuhakikisha ushindi wa kishindo kwa CCM. 

Ametumia nafasi hiyo pia kuhimiza wazazi kutoa taarifa za vitendo vya ukatili dhidi ya watoto, pamoja na kuhakikisha malezi bora kwa vijana.

“Tutakapowalea watoto wetu kwa misingi ya maadili ya kitanzania, tutajenga taifa la watu waadilifu, wanaojitambua na wanaojali utu wa wenzao,” amesema Siagi.

Maadhimisho hayo yamehusisha pia zoezi la upandaji miti katika eneo la shule ya Bunambiyu, kama ishara ya utunzaji wa mazingira na kuhimiza jamii kushiriki katika shughuli za kijani.Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mabala Mlolwa, akizungumza kwenye uzinduzi wa wiki ya Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga leo Aprili 9, 2025.Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mabala Mlolwa, akizungumza kwenye uzinduzi wa wiki ya Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga leo Aprili 9, 2025.Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mabala Mlolwa, akizungumza kwenye uzinduzi wa wiki ya Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga leo Aprili 9, 2025.Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Shinyanga John Siagi, akizungumza kwenye uzinduzi wa wiki ya wazazi leo Aprili 9, 2025.Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Shinyanga John Siagi, akizungumza kwenye uzinduzi wa wiki ya wazazi leo Aprili 9, 2025.Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Shinyanga John Siagi, akizungumza kwenye uzinduzi wa wiki ya wazazi leo Aprili 9, 2025

Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga Regina Ndulu akisoma historia ya jumuiya hiyo.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye uzinduzi wa wiki ya Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga leo Aprili 9, 2025.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye uzinduzi wa wiki ya Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga leo Aprili 9, 2025.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye uzinduzi wa wiki ya Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga leo Aprili 9, 2025.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye uzinduzi wa wiki ya Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga leo Aprili 9, 2025.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye uzinduzi wa wiki ya Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga leo Aprili 9, 2025.
Wanachama wa Jumuiya ya Wazazi, CCM na wananchi wakiwa kwenye uzinduzi wa wiki ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga leo Aprili 9, 2025 katika viwanja vya shule ya sekondari Bunambiyu Wilaya ya Kishapu.
Wanachama wa Jumuiya ya Wazazi, CCM na wananchi wakiwa kwenye uzinduzi wa wiki ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga leo Aprili 9, 2025 katika viwanja vya shule ya sekondari Bunambiyu Wilaya ya Kishapu.
Wanachama wa Jumuiya ya Wazazi, CCM na wananchi wakiwa kwenye uzinduzi wa wiki ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga leo Aprili 9, 2025 katika viwanja vya shule ya sekondari Bunambiyu Wilaya ya Kishapu.
Wanachama wa Jumuiya ya Wazazi, CCM na wananchi wakiwa kwenye uzinduzi wa wiki ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga leo Aprili 9, 2025 katika viwanja vya shule ya sekondari Bunambiyu Wilaya ya Kishapu.
Wanachama wa Jumuiya ya Wazazi, CCM na wananchi wakiwa kwenye uzinduzi wa wiki ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga leo Aprili 9, 2025 katika viwanja vya shule ya sekondari Bunambiyu Wilaya ya Kishapu.
Wanachama wa Jumuiya ya Wazazi, CCM na wananchi wakiwa kwenye uzinduzi wa wiki ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga leo Aprili 9, 2025 katika viwanja vya shule ya sekondari Bunambiyu Wilaya ya Kishapu.
Wanachama wa Jumuiya ya Wazazi, CCM na wananchi wakiwa kwenye uzinduzi wa wiki ya Wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga leo Aprili 9, 2025 katika viwanja vya shule ya sekondari Bunambiyu Wilaya ya Kishapu.
Katibu wa CCM Mkoa wa Shinyanga Odilia Batimayo akizungumza kwenye mkutano huo.
Katibu wa CCM Mkoa wa Shinyanga Odilia Batimayo akizungumza kwenye mkutano huo.
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga mjini Doris Kibabi akizungumza kwenye mkutano huo leo Aprili 9, 2025
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga mjini Mzee Fue Mrindoko akizungumza kwenye mkutano huo.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Kishapu akizungumza kwenye mkutano huo.
Viongozi mbalimbali.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Mhe. Mabala Mlolwa.
Viongozi mbalimbali.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga mjini Mhe. Anord Makombe akizungumza kwenye mkutano huo.
Viongozi mbalimbali.

Picha zote na Mapuli Misalaba

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com