Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro akikabidhi zawadi ya fedha kwa washindi wa mashindano hayo.
Na Marco Maduhu,SHINYANGA
MSHINDANO ya Katambi U-17 CUP yametamatika rasmi,huku Timu ya Katunda FC wakiibuka washindi wa michuano hiyo,baada ya kuifunga Busulwa Sec kwa mikwaju ya penati,na kisha kuondoka na Kombe pamoja na kitita cha pesa sh.milioni moja.
Fainali hiyo imechezwa Aprili 4,2025 katika Uwanja wa Chuo cha Ualimu Shinyanga SHYCOM,huku Mgeni Rasmi akiwa na Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro.
Mchezo huo umechezwa kwa kipindi cha dakika 90, na kuisha bila ya kufungana Magoli,na kisha kuchezwa mikwaju wa penati, na hatimaye Katunda FC kuibuka na ushindi wa Penati 4 kwa 3 dhidi ya Busulwa Secondari, huku mshindi wa tatu katika michuano hiyo akiibuka Ngokolo Secondari.
Mtatiro akitoa zawadi kwa washindi,amemtangaza mshindi wa Tatu ni Ngokolo Sekondari na wamepata Sh. Laki 5, Mshindi wa Pili Busulwa Sekondari sh.Laki 7, na mshindi wa kwanza Katunda FC sh,milioni 1.
Aidha, amempongeza Mbunge Katambi kwa kuendelea kuunga mkono michezo,kwamba kupitia mashindano hayo amekuwa akiibua vipaji vya vijana.
Katibu wa CCM wilaya ya Shinyanga Mjini Hamisa Chacha, amesema michezo ipo kwenye Ilani ya uchaguzi wa CCM, na kwamba Mbunge Katambi amekuwa Mbunge wa mfano kuendelea kuitekeleza Ilani hiyo, sababu michezo ni sehemu ya kuimarisha afya,kuibua vipaji pamoja na ajira.
Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu wilaya ya Shinyanga (SHIDIFA) Sylevester Budete, amempongeza Mbunge Katambi kwa kuendelea kuandaa mashindano hayo pamoja na kudhamini, huku akimuomba aendelee na jitihada hizo za kuinua michezo Shinyanga.
Nao baadhi ya vijana ambao wameshiriki mashindano hayo, wamemshukuru Katambi kwa kuonyesha vipaji vyao.
Mashindano hayo ya Katambi U-17 CUP yalizinduliwa Febuari 18,2025, na Mwenyekiti wa Jumuiya ya wazazi CCM Mkoa wa Shinyanga John Siagi, katika Uwanja wa CCM Kambarage, na kushirikisha timu 16.
TAZAMA PICHA👇👇
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro akizungumza.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro (kulia)akimkabidhi Cheti cha Pongeza Katibu wa Mbunge Katambi,Samweli Jacksoni kwa niaba ya Mbunge kwa kuendesha mashindano ya Katambi U-17 CUP kutoka SHIDIFA.
Katibu wa CCM wilaya ya Shinyanga Mjini Hamisa Chacha akizungumza.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro akikabidhi Kombe kwa Washindi wa Mashindano ya Katambi U-17 CUP kwa Kampteni wa Timu ya Katunda FC.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro akikabidhi zawadi ya fedha kwa washindi wa mashindano hayo.
Awali Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Julius Mtatiro akisalimiana na wachezaji kabla ya mechi kuanza.
Katibu wa CCM wilaya ya Shinyanga Mjini Hamisa Chacha akisalimiana na wachezaji.
Mechi ya Fainali ikiendelea kuchezwa.
Picha za pamoja na wachezaji.
Social Plugin